Na Amedeus Somi,
DAR ES SALAAM,
Akizungumza katika mkutano na wanahabari Mwenyekiti wa Taasisi ya Ayshah Sururu Foundation Bi.Aisha Sururu amesema mashindano hayo ya Kitaifa ya Quran yanatarajiwa kufanyika Aprili 2 Katika Uwanja wa Uhuru huku mgeni rasmi akitarajiwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungani wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan.
Mgeni rasmi katika Mashindano hayo anatarajiwa kuwa Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan.
Aidha Sheikh Kishki amesema mashindano makubwa ya Kimataifa ya Quran ya Dunia yanatarajiwa kufanyika Aprili 16 katika Ukumbi wa Diamond Jubilee Jijini Dar es Salaam ambapo Mgeni Rasmi anatarajiwa kuwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Uwakilishi Mhe.Dkt.Hussein Ali Mwinyi.
Naye Mstahiki Meya Wa Jiji la Dar es Salaam Mhe.Omary
Kumbilamoto amewaomba Waislam na Wtanzania kwa ujumla kujitokeza kwa wingi
katika mashindano hayo.
0 Comments