HEADLINES

6/recent/ticker-posts

WAHUDUMU WA AFYA MOI KUIMARISHA ZAIDI HUDUMA KWA WAGONJWA

 

Na Mwandishi Wetu,

DAR ES SALAAM,

Mkurugenzi Mtendaji wa MOI Prof.Abel Makubi amefanya kikao cha kimkakati na watumishi wa kada za wahudumu wa afya na huduma kwa wateja na viongozi wao  kwa lengo la kuboresha huduma kwa wateja wanaofika MOI kupata huduma.

Prof. Makubi amewapongeza wahudumu wa afya wa Taasisi ya MOI kwa kazi kubwa wanayoifanya kwani wao ni jicho la hospitali na ni sehemu kubwa katika uendeshaji wa Taasisi.

“Napenda kuwaomba idara zote tuongeze ufanisi katika kazi ili kuendelea kuboresha huduma na kuongeza mapato ambayo yataimarisha Taasisi kifedha ili kuboresha huduma zetu na uendeshaji wa hospitali" Alisema, Prof.Makubi.

 

Kwa upande mwingine Prof. Makubi amesema kwa sasa kipaumbele cha Wizara ya Afya chini ya Waziri  Ummy Mwalimu (MB)  ni ubora wa huduma  hivyo lazima tutaboreshe huduma kutoka hapa tulipo kwenda mbele zaidi ikiwa ndio ajenda ya kwanza kuliko zote kwenye sekta ya Afya.

“Inabidi tuzingatie mambo muhimu  kama salamu, kukaribisha mgonjwa, kumpa pole mgonjwa na ndugu wa mgonjwa wafikapo MOI, kumuelekeza anapotaka kufika pamoja ,kumuuliza kama anachangamoto au mahangaiko na kuondoa vitu kama chuki vilevile kuwa wepesi katika utoaji huduma ili mgonjwa asikae muda mrefu kusubiria matibabu" amesema Prof Makubi.



Aidha ,Prof.Makubi amewaomba watumishi wote  kubadilisha fikra,  kuwa na mtazamo chanya kuwa na 'Sense of ownership'  na kuzingatia maadili kama kutokupokea rushwa na kutoa taarifa potofu, kujituma vilevile utunzaji wa mali za Taasisi.

Nyinginezo

Kikao hichi ni muendelezo wa vikao baina ya Prof. Makubi na makundi mbalimbali ya watumishi kwa lengo la kuboresha huduma. Katika kikao hicho Prof Makubi amewakumbusha watumishi wote wa MOI kuhudhuria mkutano mkuu wa watumishi wote wa MOI siku ya Jumamosi tarehe 12/08/2023 katika ukumbi wa CPL Muhimbili.

Post a Comment

0 Comments