HEADLINES

6/recent/ticker-posts

KLINIKI ARDHI INAYOTEMBEA KUWAUNGANISHA WANANDOA KWA HIKI..

Na AMEDEUS SOMI,
DAR ES SALAAM.

Kliniki ya kurasimisha, kutatua na kutoa Hati imeingia katika siku ya pili katika Kata ya Bunju na mpaka sasa tayari imeshatoa hati zaidi ya elfu saba katika Jiji la Dar es Salaam.

Wakizungumza katika Kliniki hiyo iliyoandaliwa na Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Ardhi wananchi wa Bunju katika  Kata ya Wazo wameshukuru Serikali kwa kuwasaidia katika kufanikisha kuwapatia Hatimiliki za viwanja vyao.

Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Lucy Kabiemera amesema kama Wizara ya Ardhi wamekuja na kampeni maalum ya kutoa hatimiliki za pamoja (Mke na Mume) ambapo hii itasaidia kuongezeka kwa viwango vya umiliki wa ardhi kwa wanandoa.


“Baada ya kutoa hii hamasa hatimiliki walizotoa zaidi ya elfu saba kwa asilimia kumi zinamilikiwa na milki ya Pamoja yaani wanandoa”

Naibu Katibu Mkuu huyo amesema lengo la kuanzisha Kampeni hiyo ni kupunguza migogoro ya mirathi pindi mmoja anapofariki.

Amewasihi wananchi kuchukua hati ya pamoja ili kuepusha migogoro ya mirathi isitokee kwa baadae pindi mmoja  anapofariki kwani hali hii huchangia migogoro mingi ya ardhi na mirathi.

Kliniki hiyo inatarajia kuhamia katika mikoa ya Mwanza, Mbeya, Arusha na Tanga.


BOFYA HAPA KUONA VIDEO

https://www.youtube.com/watch?v=YCKmE7yIRrU

 

Post a Comment

0 Comments