HEADLINES

6/recent/ticker-posts

POGBA ASWEKA NYUMA YA NONDO MIAKA MINNE


Na AMEDEUS SOMI,
TURIN.

Kiungo wa Vibibi vizee wa Italia Juventus Paul Pogba amehukumiwa kifungo cha miaka minne kutojihusisha na mpira wa miguu kutokana na kubainika kutumia dawa za kusisimua misuli ambazo ni kinyume na sheria za soka.

Mahakama ya Kitaifa ya Kupambana na Matumizi ya Madawa ya Kulevya nchini Italia (TNA) ilikubali ombi la Ofisi ya Mwendesha Mashtaka wa Kupambana na Dawa za Kulevya la kutoa marufuku ya miaka minne - ambayo ni muda wa kawaida wa kupiga marufuku chini ya Kanuni ya Dunia ya Kupambana na Dawa za Kulevya World Anti-Doping Code (WADA).

Hukumu hiyo imekuja baada ya WADA kujiridhisha ambao wao ndio wanahusika na kufatilia masuala hayo.
hata hivyo baada ya hukumu hiyo imemshtusha kiungo huyo raia wa Ufaransa. 

Bingwa huyo wa Kombe la Dunia 2018 alianza kuchunguzwa mwaka jana mwezi Agosti


Pogba atakata rufaa dhidi ya kufungiwa katika Mahakama ya Usuluhishi wa Michezo.



Post a Comment

0 Comments